Monday, December 19, 2016
Rais Magufuli Afanya Uteuzi Wa Wakuu Wa Wilaya Wawili Na Wakurugenzi Watatu .........Nafasi ya Humphrey Polepole yachukuliwa na Kisare Makori
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, leo tarehe
19 Desemba, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 2 na Wakurugenzi 3
wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
Taarifa
iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa
Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Kisare M. Makori kuwa Mkuu wa Wilaya ya
Ubungo katika Mkoa wa Dar es Salaam.
Bw.
Kisare M. Makori anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Humphrey
Polepole ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu
ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi.
Halikadhalika, Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Avod Mmanda Herman kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mtwara iliyopo katika Mkoa wa Mtwara.
Bw.
Avod Mmanda Herman anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Khatib M.
Kazungu ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara
ya Fedha na Mipango.
Aidha,
Mhe. Rais Magufuli amemteua Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi kuwa
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga iliyopo Mkoani
Shinyanga.
Bw. Ramadhan Geodrey Mwangulumbi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Lewis Kalinjuna ambaye anastaafu kwa mujibu wa Sheria.
Mhe.
Rais Magufuli amemteua Bw Rojas John Romuli kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda iliyopo katika Mkoa wa Katavi.
Bw. Rojas John Romuli anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Ngalinda Hawamu Ahmada aliyefariki dunia hivi karibuni.
Mhe.
Rais Magufuli amemteua Bw. Rashid K. Gembe kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa
Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga iliyopo katika Mkoa wa Tanga.
Bw.
Rashid K. Gembe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Mkumbo Emmanuel
Barnabas ambaye uteuzi wake ulitenguliwa hivi karibuni.
Uteuzi
wa huu unaanza mara moja na wateule wote wanatakiwa kuripoti Makao
Makuu ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
mara wapatapo taarifa hii.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016
Monday, December 19, 2016
Wananchi 21 wafikishwa mahakamani kwa kuvamia na kufanya vurugu katika kituo cha polisi.
Jumla
ya watuhumiwa 21 akiwemo mwanamke mmoja wamefikishwa katika mahakama ya
Wilaya ya Chunya kwa kuhusika na vurugu zilizotokana na wananchi
wilayani humo kuvamia kituo cha polisi kwa lengo la kuwatoa watuhumiwa
wa mauaji ili kuwaadhibu.
Watu hao waliofikishwa mahakamani ni sehemu ya watuhumiwa 41 waliokamatwa, kati yao wanaume wakiwa 34 na wanaweke 7 baada ya vurugu zilizotokea jana na kusabababisha jumla ya watu 7 kujeruhiwa wakiwemo askari polisi wanne, na wananchi watatu huku mwananchi mmoja aliyefahamika kwa jina la AMOKE MBILINYI (25) akifariki dunia.
Taarifa
ya Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya imeeleza kuwa tukio hilo limetokea
mnamo tarehe 18.12.2016 majira ya saa 11:45 asubuhi katika Kituo cha
Polisi Makongolosi kilichopo Kata ya Makongolisi, Wilayani Chunya ambapo
kundi la wananchi walioamua kujichukulia sheria mkononi walivamia kituo
hicho cha Polisi na kufanya fujo kwa kuwarushia mawe hovyo askari.
Kwa
mujibu wa jeshi hilo, lengo la uvamizi huo ilikuwa ni kuwatoa
watuhumiwa wawili waliofahamika kwa majina ya 1. ERASTO ROBERT, mkazi wa
Kilombero na 2. BASI LINUS mkazi wa Makongolosi waliokuwa wanakabiliwa
na kosa la mauaji kwa lengo la kuwatoa nje na kuwauawa kwa kuwachoma
moto.
Aidha
wananchi hao walifunga barabara ya Chunya/Makongolosi kwa kuweka mawe
makubwa na magogo hali iliyosababisha usumbufu mkubwa wa watumiaji
wengine wa barabara hiyo.
Jeshi hilo limesema thamani ya uharibifu bado kufahamika na hali imerejea kuwa shwari
Awali
mnamo tarehe 11.12.2016 majira ya saa 23:20 katika Kitongoji cha
Manyanya, mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la JACOB BROWN Mkazi wa
Manyanya alivamiwa na watu wasiojulikana akiwa peke yake shambani kwake
na kuuawa ambapo Polisi walifanya msako na kuwakamata watu hao wawili
kwa mahojiano zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Monday, December 19, 2016
Uteuzi: Rais Dkt Magufuli ateua Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amefanya uteuzi wa Wenyeviti 7 wa Bodi za Taasisi za Serikali, na pia ameteua Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Tanzania na Mjumbe mmoja wa Baraza la Taifa la Biashara.
Taarifa iliyotolewa
leo tarehe 19 Desemba, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi
imewataja walioteuliwa kama ifuatavyo;
1. Rais Magufuli amemteua
Bw. Ali Mufuruki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Taifa
wa Dhamana ya Hifadhi ya Mazingira.
Ali Mufuruki ni Afisa Mtendaji
Mkuu wa Kampuni za Infotech Investment na Mwenyekiti wa Taasisi ya
Afrika inayojihusisha na uendelezaji wa vipaji vya uongozi katika ukanda
wa Afrika Mashariki.
2. Rais Magufuli amemteua Mhandisi
Christopher Kajolo Chiza kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa
Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade)
Mhandisi Christopher Kajolo Chiza anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Sabetha Mwambenja ambaye amemaliza muda wake.
3. Rais Magufuli amemteua Bw. Peter M. Maduki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA)
Peter M. Maduki anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Prof. Idrissa Mshoro ambaye amemaliza muda wake.
4. Rais Magufuli amemteua Dkt. Yamungu Kayandabila kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania (TIRA).
Dkt.
Yamungu Kayandabila ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi na anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Peter
Ilomo ambaye amemaliza muda wake.
5. Rais Magufuli amemteua Prof. Godwin Daniel Mjema kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Huduma za Fedha na Mikopo (UTT-MFI)
Prof.
Godwin Daniel Mjema ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na
anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Fadhili D. Mbaga ambaye
amemaliza muda wake.
6. Rais Magufuli amemteua Kepteni Ernest Mihayo Bupamba kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Chuo cha Bahari (DMI)
Kepteni Ernest Mihayo Bupamba ni Mwendesha Meli Mkuu (Principal Captain) Katika Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
7.
Rais Magufuli amemteua Dkt. Aloyce S. Hepelwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi
ya Taasisi ya Miradi ya Maendeleo ya Miundombinu (UTT-PID)
Dkt. Aloyce S. Hepewa ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. John Jingu kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi Tanzania.
Dkt. John Jingu ni Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Halikadhalika, Rais Magufuli amemteua Dkt. Rashid Adam Tamatama kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI).
Dkt. Rashid Adam Tamatama ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Pia, Rais Magufuli amemteua Bibi. Zuhura Muro kuwa Mjumbe wa Baraza la Taifa la Biashara (Tanzania National Business Council – TNBC).
Bibi. Zuhura Muro ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi inayojihusisha na huduma za ushauri wa ubora na mafunzo (Service Limited) katika ofisi zake za Dar es Salaam.
Wateule wote waliotajwa hapo juu, uteuzi wao umeanza tarehe 17 Desemba, 2016
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
19 Desemba, 2016
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni