AJTC VOICE FO VOICLESS

Jumanne, 7 Machi 2017

MICHEZO YA JUMANNE HII YA LEO 07/03/2017

 

TFF – KAMATI YA UTENDAJI MACHI 26, ROBO FAINALI MACHI 18!


PRESS RELEASE NO. 264                                      MACHI 7, 2017
KIKAO CHA KAMATI YA UTENDAJI TFF
Kikao cha kawaida cha Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kinatarajiwa kukaa Machi 26, mwaka huu ambako pamoja na ajenda nyingine, itaamua tarehe rasmi ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika baadaye mwaka huu.
Kikao hiki cha kawaida, kwa mujibu wa katiba hufanyika mara nne kwa mwaka na huamua masuala mbalimbali ya uendeshaji na usimamizi wa mpira wa miguu nchini.
Kadhalika Mkutano Mkuu wa uchaguzi kwa mujibu wa Katiba ya TFF, hufanyika kila baada ya miaka minne kwa mwaka.
ROBO FAINALI AZAM SPORTS FEDERATION CUP
Mechi mbili za kwanza hatua ya Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Azam (Azam Sports Sports Federation Cup 2016/2017), zitachezwa Machi 18, mwaka huu kwenye viwanja viwili tofauti.
Mechi hizo ni kati ya Kagera Sugar itakayocheza na Mbao FC ya Mwanza kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba mkoani Kagera kadhalika Simba itakayosafiri hadi Arusha kucheza na Madini kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha.
Mechi nyingine zitapangiwa tarehe za baadaye. Mechi hizo ni kati ya Azam FC na Ndanda FC kadhalika Tanzania Prisons ya Mbeya itakayocheza na mshindi kati ya Young Africans ya Dar es Salaam na Kiluvya United ya Pwani.
Bingwa wa michuano hiyo kwa mujibu wa kanuni, atazawadiwa Tsh. 50 milioni.
Pia bingwa wa michuano hiyo, ndiye atakayeiwakilisha nchi kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika ya Total wakati Bingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara ndiye ataiwakilisha nchi kwenye michuano ya Total Ligi ya Mabingwa Afrika.
..…………………………………………………………………………........................
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)  


IBRAHIMOVIC, MINGS KITANZINI.

MSHAMBULIAJI wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic na beki wa Bournemouth Tyrone Mings wamefunguliwa Mashitaka na Chama Soka cha Uingereza-FA kwa kuonyesha mchezo usio wa kiungwana. Wachezaji hao walichezeana faulo mara kwa mara kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya Ligi Kuu ambapo timu hizo zilitoka Sare 1-1 katika Uwanja wa Old Trafford. Mings alimchezea faulo kwa kumkanyaga kichwani Ibrahimovic aliyekuwa ameanguka chini katika dakika ya 44 na dakika 2 baadae Ibrahimovic alijibu kwa kumpiga kiwiko Mings wakati akipiga kichwa mpira wa kona. Wachezaji hao wamepewa muda hadi kufikia leo kujibu mashitaka yao, FA imeeleza Matukio hayo waliyoshitakiwa nayo hayakuonwa na mwamuzi Kevin Friend lakini yalinaswa kwenye picha za video wakati mchezo ukiendelea. Kwa mujibu wa kanuni za FA, mchezaji kumpiga kiwiko na kumkanyaga mchezaji mwezake kwa makusudi ni faulo ambazo zinastahili kutolewa kadi nyekundu na pia adhabu ya kutocheza mechi tatu.

GUARDIOLA AELEZA MIPANGO YA USAJILI KIANGAZI.

MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema klabu inajipanga kufanya usajili majira ya kiangazi na wanakusudia kusajili wachezaji chipukizi wenye vipaji. City wako kwenye hatua za katikati katika mipango yao ya kusuka kikosi chao kufuatia kuwasajili John Stones, Claudio Bravo, Leroy Sane, Ilkay Gundogan, Nolito na Gabriel Jesus kiangazi mwaka jana. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Guardiola amesema klabu inasajili kwa ajili ya mipango ya muda mrefu ndio maana wamekuwa na wachezaji kama Raheem Sterling, Jesus na Sane. Guardiola amesema wanaweza kuongeza mchezaji mmoja au wawili wenye umri mkubwa kwsababu ya uzoefu pindi dirisha la usajili likapofunguliwa Juni.

XAVI ATAMANI KUINOA BARCELONA.

NGULI wa soka wa zamani wa Barcelona, Xavi amedai ana ndoto za kuja kuinoa klabu hiyo lakini ameweka wazi kuwa hayuko katika mpango wa kuchukua nafasi ya Luis Enrique mwishoni mwa msimu huu. Enrique alibainisha wiki iliyopita kuwa taachia ngazi pindi msimu utakapokamilika baada ya kukaa Camp Nou kwa miaka mitatu huku baadhi ya watu wakimpigia chapuo Xavi kuwa mtu sahihi wa kuchukua nafasi hiyo. Hata hivyo, pamoja na kwamba nguli huyo mwneye umri wa miaka 37 anayecheza soka katika timu ya Al Sadd ya Qatar, anapenda kuja kuinoa Barcelona siku za usoni lakini ameondoa uwezekano wa kutua sasa hivi kwakuwa hana uzoefu wa kutosha bado. Xavi amesema bado kuna vingi vya kujifunza pale linapokuja suala la kuwaongoza wachezaji 25 na benchi zima la ufundi pamoja na madaktari.

CONTE AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUTOLEWA SIFA.

MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amewataka wachezaji wake kutulia baada ya kuifunga West Ham United kwa mabao 2-1 jana na kupiga hatua kubwa kuelekea katika ubingwa wa ligi Kuu. Chelsea wanaongoza kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshika nafasi ya pili huku kukiwa kumebaki mechi 11 kabla ya msimu kumalizika. Mashabiki wa klabu hiyo jana walikuwa wakiimba nyimbo za ubingwa katika London, lakini Conte amesema wanapaswa kufikia jinsi ya kuchukua alama 26 zilizobakia kabla ya kujitangaza mabingwa. Akizungumza na wanahabari, Conte amesema wanapaswa kufikiri kila mpinzani watakayekutana naye anataka kuwafunga kuanzia sasa mpaka mwishoni. Conte aliendelea kudai kuwa mpaka sasa walipofika ni pazuri lakini jambo la muhimu ni kutojisahau na kuhakikisha wanaendeleza makal
IBRAHIMOVIC, MINGS KITANZINI. MSHAMBULIAJI wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic na beki wa Bournemouth Tyrone Mings wamefunguliwa Mashitaka na Chama Soka cha Uingereza-FA kwa kuonyesha mchezo usio wa kiungwana. Wachezaji hao walichezeana faulo mara kwa mara kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya Ligi Kuu ambapo timu hizo zilitoka Sare 1-1 katika Uwanja wa Old Trafford. Mings alimchezea faulo kwa kumkanyaga kichwani Ibrahimovic aliyekuwa ameanguka chini katika dakika ya 44 na dakika 2 baadae Ibrahimovic alijibu kwa kumpiga kiwiko Mings wakati akipiga kichwa mpira wa kona. Wachezaji hao wamepewa muda hadi kufikia leo kujibu mashitaka yao, FA imeeleza Matukio hayo waliyoshitakiwa nayo hayakuonwa na mwamuzi Kevin Friend lakini yalinaswa kwenye picha za video wakati mchezo ukiendelea. Kwa mujibu wa kanuni za FA, mchezaji kumpiga kiwiko na kumkanyaga mchezaji mwezake kwa makusudi ni faulo ambazo zinastahili kutolewa kadi nyekundu na pia adhabu ya kutocheza mechi tatu. Posted by beki3 at 4:35 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest GUARDIOLA AELEZA MIPANGO YA USAJILI KIANGAZI. MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema klabu inajipanga kufanya usajili majira ya kiangazi na wanakusudia kusajili wachezaji chipukizi wenye vipaji. City wako kwenye hatua za katikati katika mipango yao ya kusuka kikosi chao kufuatia kuwasajili John Stones, Claudio Bravo, Leroy Sane, Ilkay Gundogan, Nolito na Gabriel Jesus kiangazi mwaka jana. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Guardiola amesema klabu inasajili kwa ajili ya mipango ya muda mrefu ndio maana wamekuwa na wachezaji kama Raheem Sterling, Jesus na Sane. Guardiola amesema wanaweza kuongeza mchezaji mmoja au wawili wenye umri mkubwa kwsababu ya uzoefu pindi dirisha la usajili likapofunguliwa Juni. Posted by beki3 at 4:18 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest XAVI ATAMANI KUINOA BARCELONA. NGULI wa soka wa zamani wa Barcelona, Xavi amedai ana ndoto za kuja kuinoa klabu hiyo lakini ameweka wazi kuwa hayuko katika mpango wa kuchukua nafasi ya Luis Enrique mwishoni mwa msimu huu. Enrique alibainisha wiki iliyopita kuwa taachia ngazi pindi msimu utakapokamilika baada ya kukaa Camp Nou kwa miaka mitatu huku baadhi ya watu wakimpigia chapuo Xavi kuwa mtu sahihi wa kuchukua nafasi hiyo. Hata hivyo, pamoja na kwamba nguli huyo mwneye umri wa miaka 37 anayecheza soka katika timu ya Al Sadd ya Qatar, anapenda kuja kuinoa Barcelona siku za usoni lakini ameondoa uwezekano wa kutua sasa hivi kwakuwa hana uzoefu wa kutosha bado. Xavi amesema bado kuna vingi vya kujifunza pale linapokuja suala la kuwaongoza wachezaji 25 na benchi zima la ufundi pamoja na madaktari. Posted by beki3 at 4:15 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest CONTE AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUTOLEWA SIFA. MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amewataka wachezaji wake kutulia baada ya kuifunga West Ham United kwa mabao 2-1 jana na kupiga hatua kubwa kuelekea katika ubingwa wa ligi Kuu. Chelsea wanaongoza kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshika nafasi ya pili huku kukiwa kumebaki mechi 11 kabla ya msimu kumalizika. Mashabiki wa klabu hiyo jana walikuwa wakiimba nyimbo za ubingwa katika London, lakini Conte amesema wanapaswa kufikia jinsi ya kuchukua alama 26 zilizobakia kabla ya kujitangaza mabingwa. Akizungumza na wanahabari, Conte amesema wanapaswa kufikiri kila mpinzani watakayekutana naye anataka kuwafunga kuanzia sasa mpaka mwishoni. Conte aliendelea kudai kuwa mpaka sasa walipofika ni pazuri lakini jambo la muhimu ni kutojisahau na kuhakikisha wanaendeleza makali yao.

Cheap Offers: http://bit.ly/gadgets_cheap
IBRAHIMOVIC, MINGS KITANZINI. MSHAMBULIAJI wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic na beki wa Bournemouth Tyrone Mings wamefunguliwa Mashitaka na Chama Soka cha Uingereza-FA kwa kuonyesha mchezo usio wa kiungwana. Wachezaji hao walichezeana faulo mara kwa mara kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya Ligi Kuu ambapo timu hizo zilitoka Sare 1-1 katika Uwanja wa Old Trafford. Mings alimchezea faulo kwa kumkanyaga kichwani Ibrahimovic aliyekuwa ameanguka chini katika dakika ya 44 na dakika 2 baadae Ibrahimovic alijibu kwa kumpiga kiwiko Mings wakati akipiga kichwa mpira wa kona. Wachezaji hao wamepewa muda hadi kufikia leo kujibu mashitaka yao, FA imeeleza Matukio hayo waliyoshitakiwa nayo hayakuonwa na mwamuzi Kevin Friend lakini yalinaswa kwenye picha za video wakati mchezo ukiendelea. Kwa mujibu wa kanuni za FA, mchezaji kumpiga kiwiko na kumkanyaga mchezaji mwezake kwa makusudi ni faulo ambazo zinastahili kutolewa kadi nyekundu na pia adhabu ya kutocheza mechi tatu. Posted by beki3 at 4:35 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest GUARDIOLA AELEZA MIPANGO YA USAJILI KIANGAZI. MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema klabu inajipanga kufanya usajili majira ya kiangazi na wanakusudia kusajili wachezaji chipukizi wenye vipaji. City wako kwenye hatua za katikati katika mipango yao ya kusuka kikosi chao kufuatia kuwasajili John Stones, Claudio Bravo, Leroy Sane, Ilkay Gundogan, Nolito na Gabriel Jesus kiangazi mwaka jana. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Guardiola amesema klabu inasajili kwa ajili ya mipango ya muda mrefu ndio maana wamekuwa na wachezaji kama Raheem Sterling, Jesus na Sane. Guardiola amesema wanaweza kuongeza mchezaji mmoja au wawili wenye umri mkubwa kwsababu ya uzoefu pindi dirisha la usajili likapofunguliwa Juni. Posted by beki3 at 4:18 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest XAVI ATAMANI KUINOA BARCELONA. NGULI wa soka wa zamani wa Barcelona, Xavi amedai ana ndoto za kuja kuinoa klabu hiyo lakini ameweka wazi kuwa hayuko katika mpango wa kuchukua nafasi ya Luis Enrique mwishoni mwa msimu huu. Enrique alibainisha wiki iliyopita kuwa taachia ngazi pindi msimu utakapokamilika baada ya kukaa Camp Nou kwa miaka mitatu huku baadhi ya watu wakimpigia chapuo Xavi kuwa mtu sahihi wa kuchukua nafasi hiyo. Hata hivyo, pamoja na kwamba nguli huyo mwneye umri wa miaka 37 anayecheza soka katika timu ya Al Sadd ya Qatar, anapenda kuja kuinoa Barcelona siku za usoni lakini ameondoa uwezekano wa kutua sasa hivi kwakuwa hana uzoefu wa kutosha bado. Xavi amesema bado kuna vingi vya kujifunza pale linapokuja suala la kuwaongoza wachezaji 25 na benchi zima la ufundi pamoja na madaktari. Posted by beki3 at 4:15 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest CONTE AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUTOLEWA SIFA. MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amewataka wachezaji wake kutulia baada ya kuifunga West Ham United kwa mabao 2-1 jana na kupiga hatua kubwa kuelekea katika ubingwa wa ligi Kuu. Chelsea wanaongoza kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshika nafasi ya pili huku kukiwa kumebaki mechi 11 kabla ya msimu kumalizika. Mashabiki wa klabu hiyo jana walikuwa wakiimba nyimbo za ubingwa katika London, lakini Conte amesema wanapaswa kufikia jinsi ya kuchukua alama 26 zilizobakia kabla ya kujitangaza mabingwa. Akizungumza na wanahabari, Conte amesema wanapaswa kufikiri kila mpinzani watakayekutana naye anataka kuwafunga kuanzia sasa mpaka mwishoni. Conte aliendelea kudai kuwa mpaka sasa walipofika ni pazuri lakini jambo la muhimu ni kutojisahau na kuhakikisha wanaendeleza makali yao.

Cheap Offers: http://bit.ly/gadgets_cheap

LEO ARSENAL KUIAGA RASMI ULAYA? WANAWEZA KUPINDUA KIPONDO CHA 5-1 CHA BAYERN?


KWA MARA NYINGINE tena Arsenal wanachungulia kutupwa nje ya Hatua ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, hatua ambayo mara ya mwisho waliivuka Msimu wa 2009/10.
Kibarua kigumu cha Arsenakl kinatokana na kuchapwa 5-1 na Wababe wa Germany Bayern Munich kwenye Mechi yao ya Kwanza iliyochezwa Allianz Arena huko Munich.
Ili kusonga Robo Fainali, Arsenal wanahitaji ushindi wa 4-0 au matokeo mengine ili mradi tofauti ya Magoli ibakie 4-0 kwa upande wao.
Kazi hii ngumu ipo ngumu zaidi kwao kwa vile pia watamkosa Kiungo wao Mjerumani Mesut Ozil ambae ni Mgonjwa.
Lakini Arsenal wanaweza kumtumia kwa mara ya kwanza Sentahafu wao Mjerumani Per Mertesacker ambae ni Kepteni wao baada ya kupona Goti na hii itakuwa Mechi yake ya kwanza kucheza Msimu huu ikiwa atacheza.
Pia huenda Meneja wa Arsenal Arsene Wenger huenda akamuanzisha Fowadi wao kutoka Chile Alexis Sanchez ambae hakuanza Jumamosi iliyopita walipotwangwa 3-1 na Liverpool huko Anfield kwenye Mechi ya Ligi Kuu England baada kuvumishwa kulikuwa na rabsha Mazoezini iliyomhusu yeye.
Sanchez ndie Mfungaji Bora wa Arsenal Msimu huu akiwa na Bao 20.
Kwa upande wa Bayern Munich, chini ya Kocha Mtaliano Carlo Ancelotti, itawakosa Jerome Boateng ambae ni Majeruhi na Philipp Lahm ambae yupo Kifungoni.
+++++++++
JE WAJUA?
-Arsenal na Bayern zimekutana mara 11 na 7 kati ya hizo ni katika Miaka Minne iliyopita.
-Bayern imeshinda Mechi 6 na kufungwa 3 tu kati ya hizo huku wakiipiga Arsenal 5-1 mara 2 mfululizo katika Mechi 2 zilizopita.
-Hakuna Klabu iliyowahi kupindua kipigo cha Bao 4-0 au zaidi katika Mechi ya Kwanza na kusonga kwenye UCL.
+++++++++
Pengine matumaini makubwa kwa Arsenal ni kuwa Bayern imepigwa mara 2 mfululizo kila walipotua England katika Mechi 2 zilizopita na ya mwisho ikiwa Emirates walipochapwa 2-0 na Arsenal kwa Bao za Olivier Giroud na Mesut Ozil.
Lakini Bayern watatua Emirates wakiwa hawajafungwa katika Mechi 16 huku wakishinda Mechi 14 kati ya hizo mbio zilizoanzia Novemba Mwaka Jana.
Katika Mechi zao 5 zilizopita, Bayern wamenyuka Bao 20.
VIKOSI VINATARAJIWA KUWA:
ARSENAL: Ospina; Bellerin, Koscielny, Mustafi, Gibbs; Ramsey, Xhaka, Walcott, Iwobi, Sanchez; Giroud
BAYERN MUNICH: Neuer; Rafinha, Martinez, Hummels, Alaba; Alonso, Kimmich, Ribery, Muller, Robben; Lewandowski
REFA: Tasos Sidiropoulos (Greece)
UEFA CHAMPIONZ LIGI
Raundi ya Mtoano ya Timu 16
**Mechi zote kuanza Saa 4 Dakika 45 Usiku Saa za Bongo
Mechi za Pili
**Kwenye Mabano Matokeo Mechi za Kwanza
Jumanne 14 Machi 2017
Juventus v FC Porto      [2-0]
Leicester City v Sevilla [1-2]           
Jumatano 15 Machi 2017
Atlético Madrid v Bayer 04 Leverkusen [4-2]              
Monaco v Manchester City [3-5]     
++++++++++++++++++++++++++++
TAREHE MUHIMU:
MECHI ZA MTOANO:
14/15 na 21/22 Feb 2017: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Mechi ya Kwanza
7/8 na 14/15 Machi 2017: Raundi ya Mtoano ya Timu 16, Mechi ya Pili
11–12/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Kwanza
18–19/04/17: Robo Fainali, Mechi ya Pili
02–03/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Kwanza
09–10/05/17: Nusu Fainali, Mechi ya Pili
03/06/17: Fainali (National Stadium of Wales, Cardiff)

CHELSEA YAPIGA, YAELEKEA UBINGWA!


    
++++++++++++++++++++
CHELSEA-UBINGWA
VINARA wa EPL, Ligi Kuu England, Chelsea, Jana wamezidi kupaa kileleni na sasa kuwa Pointi 10 mbele ya Timu ya Pili Tottenham Hotspur baada ya kuichapa West Ham United 2-1 huko London Stadium Jijini London.
Sasa, baada ya Mechi 27, Chelsea wana Pointi 66, Tottenham na wa 3 ni Man City wenye Pointi 55 kwa Mechi 26.
Hadi Mapumziko Chelsea walikuwa mbele 1-0 kwa Bao la Dakika ya 25 la Eden Hazard baada ya N'Golo Kante kuinasa Pasi ya Mchezaji wa West Ham Robert Snodgrass upande wa Chelsea na kumpasia Hazard aliesonga mbele na kucheza moja mbili na Pedro na kisha kumchambua Kipa Darren Randolph na kufunga.
Bao la Pili la Chelsea lilifungwa na Diego Costa katika Dakika ya 50 akiunganisha Kona ya Hazard na hilo ni Bao lake la 17 la Ligi Msimu huu.
West Ham walipata Bao lao pekee Dakika za Majeruhi, Dakika ya 92, baada ya Andy Carroll kumnyang’anya Mpira Cesc Fabregas na kumlisha Andrew Ayew aliempasia Lanzini na kufunga.
Ushindi huu ni wa 21 kwa Chelsea kwenye EPL Msimu huu na kidogo kidogo wananyemelea Utepe wa kutwaa Ubingwa.EPL-MAR7
VIKOSI:
West Ham:Randolph, Kouyate, Fonte, Reid [Byram 64'], Cresswell, Obiang, Noble [Fernandes 77'], Feghouli [Ayew 64'], Lanzini, Snodgrass, Carroll
Akiba:Adrian, Collins, Masuaku, Byram, Fernandes, Ayew, Calleri.
Chelsea:Courtois, Azpilicueta, David Luiz, Cahill, Moses [Zouma 76'], Fabregas, Kante, Alonso, Pedro [Matic 65'], Costa, Hazard [Willian 75']
Akiba:Begovic, Terry, Zouma, Matic, Loftus-Cheek, Willian, Batshuayi.
REFA:Andre Marriner
EPL – Ligi Kuu England
Ratiba
Jumamosi Machi 11
1800 Bournemouth v West Ham United           
Crystal Palace v Tottenham Hotspur [IMEAHIRISHWA]
1800 Everton v West Bromwich Albion            
1800 Hull City v Swansea City     
Middlesbrough v Sunderland [IMEAHIRISHWA]
Arsenal v Leicester City [IMEAHIRISHWA]
Jumapili Machi 12
Southampton v Manchester United [IMEAHIRISHWA]
1900 Liverpool v Burnley            
Jumatatu Machi 13
Chelsea v Watford [IMEAHIRISHWA]
Jumamosi Machi 18
1530 West Bromwich Albion v Arsenal             
1800 Crystal Palace v Watford              
1800 Everton v Hull City             
1800 Stoke City v Chelsea          
1800 Sunderland v Burnley         
1800 West Ham United v Leicester City 
2030 Bournemouth v Swansea City                 
Jumapili Machi 19
1500 Middlesbrough v Manchester United                 
1715 Tottenham Hotspur v Southampton                  
1930 Manchester City v Liverpool       

   

CHIRWA AFUNGA NNE, YANGA YAWAJERUHI KILUVYA 6-1 KOMBE LA TFF


YANGA SC imefanikiwa kwenda Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa ushindi wa kishindo wa mabao 6-1 dhidi ya Kiluvya United ya Pwani katika mchezo wa kukamilisha hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo inayojulikana pia kama Azam Sports Federation Cup (ASFC).
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, mshambuliaji Mzambia Obrey Chirwa alifunga mabao manne peke yake, huku mengine yakifungwa na viungo Geoffrey Mwashiuya na Juma Mahadhi. 
Yanga sasa itamenyana na Prisons katika Robo Fainali Machi 18, mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mzambia Obrey Chirwa amefunga mabao manne peke yake, Yanga ikiichapa Kiluvya United 6-1 

Robo fainali nyingine zitakuwa kati ya Simba SC na Madini FC Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha, Azam FC na Ndanda FC ya Mtwara Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam na Kagera Sugar na Mbao FC ya Mwanza Uwanja wa Kaitaba.  
Katika mchezo wa leo uliochezeshwa refa hodari anayechipukia nchini, Kheri Sasii, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-1.
Winga Geoffrey Mwashiuya alianza kuwafungia Yanga bao la kwanza dakika ya 11 kwa shuti kali baada ya kuwatoka vizuri wachezaji wa Kiluvya United kuanzia katikati pembezoni mwa Uwanja kushoto kufuatia pasi ya beki wa kushoto, Oscar Joshua.
⁠⁠⁠mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa akaifungia Yanga bao la pili dakika ya 24 kwa shuti kali pia baada ya pasi nzuri ya kutanguliziwa na mshambuliaji pacha wake leo, Juma Mahadhi. 
Chipukizi Edgar Charles Mfumakule akamtoka vizuri beki Mtogo, Vincent Bossou baada ya pasi ya Shala Juma na kumtungua kipa Deogratius Munishi ‘Dida’ kuipatia Kiluvya United bao la kufutia machozi.
Geoffrey Mwashiuya na Juma Mahadhi walifunga mabao mengine ya Yanga leo
Juma Mahadhi (kushoto) aliumia misuli baada ya kufunga bao la tano dakika ya 74 na hakuweza kurejea uwanjani

Chirwa akaifungia Yanga mabao mawili mfulilizo dakika za 45 akimalizia pasi ya Juma Mahadhi na dakika ya 70 akimalizia krosi ya Hassan Kessy kukamilisha hat trick yake ya kwanza tangu ajiunge na timu hiyo Julai mwaka jana kutoka FC Platinums ya Zimbabwe.
Juma Mahadhi akaifungia Yanga bao la tano dakika ya 74 kwa shuti la umbali wa mita 21 hadi misuli ikambana. Yanga ilicheza pungufu tangu dakika ya 74 baada ya Mahadhi kuumia misuli na kutoka nje, wakati wamekwishatimiza idadi ya wachezaji watatu wa kubadili.
Kikosi cha Yanga kilikuwa; Deogratias Munishi ‘Dida’, Hassan Kessy, Oscar Joshua, Vincent Bossou, Said Juma ‘Makapu’/Justin Zulu dk48, Yussuf Mhilu/Emmanuel Martin dk35, Deus Kaseke, Juma Mahadhi, Obrey Chirwa na Geoffrey Mwashiuya/Simon Msuva dk44. 
Kiluvya United: Philimoni Ramadhani, Nassor Abubakar/Hashik Fakhi dk62, Ramadhani Ally, Jagani Mvugalo, Aloyce Nkya, Mwita Emmanuel, Yohana Richard, Hassan Ayoub, Edgar Charles/Juma Mohammed dk79, Shala Juma na Mwinyi Rehani/Ramadhani Said dk79.
 

KIINGILIO CHA CHINI AZAM NA MBABANE 3,000 TU


KIINGILIO cha chini katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Afrikaa kati ya wenyeji, Azam FC na Mbabane Swallows ya Swaziland Jumapili wiki hii kitakuwa Sh. 3,000.
Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam kuanzia Saa 1.15 usiku.
Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd Maganga amesema leo mjini Dar es Salaam kwamba Sh. 3000 ni kwa mashabiki watakaoketi majukwaa ya mzunguko.
Maganga amesema eneo la V.I.P B kiingilio kitakuwa ni Sh. 5,000 na V.I.P A itakuwa Sh. 10,000 na mashabiki watanunua tiketi kwa njia ya mtandao kupitia kampuni ya Selcom.
Nahodha wa Azam FC, John Bocco (kulia) anatarajiwa kuwa fiti kwa mchezo dhidi ya Mbabane
Maganga amesema wameamua kuuza tiketi hizo mapema, ili kuwarahisishia mashabiki wa soka nchini kupata tiketi hizo kwa haraka na kutosumbuka watakapokuwa wamefunga safari yao kuja kushuhudia mchezo huo.
“Kama unavyojua uwanja wetu ni mdogo, hivyo kwa kuuza tiketi hizo kwa mfumo huo tutakuwa tumewapunguzia usumbufu mashabiki wa soka kwani idadi kamili ikishatimia ya mashabiki wanaotakiwa basi zoezi la uuzaji tiketi litahitimishwa,” alisema.
Aidha alitoa wito kwa mashabiki kununua tiketi zao mapema ili kujiwekea uhakika wa kushuhudia uhondo wa mchezo huo kwani hadi sasa watu wengi wamekuwa na shauku kubwa ya kujitokeza uwanjani.
Katika hatua nyingine, waamuzi watakaochezesha mchezo huo kutoka nchini Benin wanatarajiwa kuwasili nchini Ijumaa hii, ambao ni Mwamuzi wa Kati Adissa Abdul Raphiou Ligali, Mwamuzi Msaidizi Namba Moja, Medegnonwa Romains Agbodjogbe huku Msaidizi Namba Mbili akiwa ni Babadjide Bienvenu Dina. 
Kikosi cha Azam FC, kinachodhaminiwa na kinywaji safi cha Azam Cola burudani kwa koo lako na Benki bora kabisa nchini ya NMB, kipo kwenye hali nzuri kuelekea mchezo huo kikiwa hakika majeruhi hata mmoja jambo ambalo linatia matumaini makubwa ya timu hiyo kupata matokeo mazuri.
Jambo pekee ambalo limebakia hivi sasa, ni mashabiki wa soka kwa ujumla wenu nchini hasa jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kuipa sapoti Azam FC kwenye mchezo huo kwani ndio moja ya timu pamoja na Yanga, ambazo zinaiwakilisha Tanzania Bara katika michuano ya Afrika.

IBRAHIMOVIC, MINGS KITANZINI. MSHAMBULIAJI wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic na beki wa Bournemouth Tyrone Mings wamefunguliwa Mashitaka na Chama Soka cha Uingereza-FA kwa kuonyesha mchezo usio wa kiungwana. Wachezaji hao walichezeana faulo mara kwa mara kwenye mechi ya Jumamosi iliyopita ya Ligi Kuu ambapo timu hizo zilitoka Sare 1-1 katika Uwanja wa Old Trafford. Mings alimchezea faulo kwa kumkanyaga kichwani Ibrahimovic aliyekuwa ameanguka chini katika dakika ya 44 na dakika 2 baadae Ibrahimovic alijibu kwa kumpiga kiwiko Mings wakati akipiga kichwa mpira wa kona. Wachezaji hao wamepewa muda hadi kufikia leo kujibu mashitaka yao, FA imeeleza Matukio hayo waliyoshitakiwa nayo hayakuonwa na mwamuzi Kevin Friend lakini yalinaswa kwenye picha za video wakati mchezo ukiendelea. Kwa mujibu wa kanuni za FA, mchezaji kumpiga kiwiko na kumkanyaga mchezaji mwezake kwa makusudi ni faulo ambazo zinastahili kutolewa kadi nyekundu na pia adhabu ya kutocheza mechi tatu. Posted by beki3 at 4:35 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest GUARDIOLA AELEZA MIPANGO YA USAJILI KIANGAZI. MENEJA wa Manchester City, Pep Guardiola amesema klabu inajipanga kufanya usajili majira ya kiangazi na wanakusudia kusajili wachezaji chipukizi wenye vipaji. City wako kwenye hatua za katikati katika mipango yao ya kusuka kikosi chao kufuatia kuwasajili John Stones, Claudio Bravo, Leroy Sane, Ilkay Gundogan, Nolito na Gabriel Jesus kiangazi mwaka jana. Akizungumza na wanahabari kuhusiana na suala hilo, Guardiola amesema klabu inasajili kwa ajili ya mipango ya muda mrefu ndio maana wamekuwa na wachezaji kama Raheem Sterling, Jesus na Sane. Guardiola amesema wanaweza kuongeza mchezaji mmoja au wawili wenye umri mkubwa kwsababu ya uzoefu pindi dirisha la usajili likapofunguliwa Juni. Posted by beki3 at 4:18 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest XAVI ATAMANI KUINOA BARCELONA. NGULI wa soka wa zamani wa Barcelona, Xavi amedai ana ndoto za kuja kuinoa klabu hiyo lakini ameweka wazi kuwa hayuko katika mpango wa kuchukua nafasi ya Luis Enrique mwishoni mwa msimu huu. Enrique alibainisha wiki iliyopita kuwa taachia ngazi pindi msimu utakapokamilika baada ya kukaa Camp Nou kwa miaka mitatu huku baadhi ya watu wakimpigia chapuo Xavi kuwa mtu sahihi wa kuchukua nafasi hiyo. Hata hivyo, pamoja na kwamba nguli huyo mwneye umri wa miaka 37 anayecheza soka katika timu ya Al Sadd ya Qatar, anapenda kuja kuinoa Barcelona siku za usoni lakini ameondoa uwezekano wa kutua sasa hivi kwakuwa hana uzoefu wa kutosha bado. Xavi amesema bado kuna vingi vya kujifunza pale linapokuja suala la kuwaongoza wachezaji 25 na benchi zima la ufundi pamoja na madaktari. Posted by beki3 at 4:15 AM No comments: Email ThisBlogThis!Share to TwitterShare to FacebookShare to Pinterest CONTE AWATAKA WACHEZAJI WAKE KUTOLEWA SIFA. MENEJA wa Chelsea, Antonio Conte amewataka wachezaji wake kutulia baada ya kuifunga West Ham United kwa mabao 2-1 jana na kupiga hatua kubwa kuelekea katika ubingwa wa ligi Kuu. Chelsea wanaongoza kwa tofauti ya alama 10 dhidi ya Tottenham Hotspurs wanaoshika nafasi ya pili huku kukiwa kumebaki mechi 11 kabla ya msimu kumalizika. Mashabiki wa klabu hiyo jana walikuwa wakiimba nyimbo za ubingwa katika London, lakini Conte amesema wanapaswa kufikia jinsi ya kuchukua alama 26 zilizobakia kabla ya kujitangaza mabingwa. Akizungumza na wanahabari, Conte amesema wanapaswa kufikiri kila mpinzani watakayekutana naye anataka kuwafunga kuanzia sasa mpaka mwishoni. Conte aliendelea kudai kuwa mpaka sasa walipofika ni pazuri lakini jambo la muhimu ni kutojisahau na kuhakikisha wanaendeleza makali yao.

Cheap Offers: http://bit.ly/gadgets_cheap

Ijumaa, 10 Februari 2017

HABARI ZA MICHEZO JUAMOSI YA TAREHE 11/02/2017

Mkuu wa Mkoa ameikatia ‘fungu’ Singida United ipande ligi kuu



Katika kuongeza hamasa kwa wachezaji wa Singida United, mkuu wa mkoa huo Dkt. Rehema Nchimbiameibuka kwenye kambi ya timu na kutoa kiasi cha shilingi 500,000 kama hamasa ya kuhakikisha timu inapata ushindi.
“Mimi ninawafahamu wanangu kwamba mnaweza, hiyo 500,000 niliyowapa ni sadaka ili mtuombee kwa Mungu viongozi wenu na watendaji wote.” – Dkt. Rehema Nchimbi
“Sasa ninatoa sadaka ili mtuombee kwa Mungu atusamehe ili uwepo wake uwepo ili tuweze kuvuka vizuri.”


Singida United vs Alliance hadi kieleweke VPL



Macho na masikio ya watanzania yapo kwenye mechi ambayo itapigwa kwenye uwanja wa Namfua mkoani Singida kati ya Singida United dhidi ya Alliance Academy ya Mwanza mchezo wa ligi daraja la kwanza Tanzania bara Kundi C.
Kocha wa Alliance Salvatory Edward amesema vijana wake wapo vizuri na wanataraji wakuwashangaza wakazi wote wa Singida pamoja na wananchi wa maeneo jirani.
“Vijana wote wako tayari kwa ajili ya mchezo dhidi ya Singida United ambao ni mgumu ukizingatia kila timu ina nafasi ya kwenda ligi kuu, majeruhi ni wachache sana lakini kwa ujumla vijana wako vizuri.”
Kocha wa Singina Unidted Fred Felix Minziro amsema, kila mkazi wa Singida aende uwanjani kushuhudia timu yao inavyokata tiketi ya kufuzu kucheza ligi kuu.
Kwa ujumla maandalizi yanakweda vizuri hakuna majeruhi yeyote, tumejipanga kupambana kama unavyojua mechi hiyo ni kufa au kupona lakini sisi tumejipanga kuhakikisha watu wa Singida angalau wanapata timu inayocheza ligi kuu.
Morali ipo juu kwa sababu watu wa Singida wana hamu ya kuona timu yao inacheza ligi kuu baada ya kukosa kwa miaka 17.
Nawaheshimu Alliance ni timu nzuri lakini na sisi tumejipanga kukabiliana na hilo kwa sababu walitufunga kwenye mchezo wa kwanza nyumbani kwao kwa hiyo na sisi tunataka kulipa kisasi.
Mechi nyingine za Kundi C ligi daraja la kwanza
Mgambo Shooting va Polisi Dodoma
Polisi Mara vs Mvuvumwa FC
Panone FC vs Rhino Rangers
Mechi za Kundi B
Mlale JKT vs Kurugenzi FC
Njombe Mji vs Coastal Union


‘Ondoeni shaka, kila kitu kipo kwenye mstari’ – Mkwasa





Katibu Mkuu wa Young Africans Charles Boniface Mkwasa amesema tayari wameshakamilisha taratibu zote za safari kuelekea visiwani Comoro kwa ajili ya mchezo wao wa klabu bingwa Afrika dhidi ya Ngaya Club.
“Maandalizi yote yamekamilika kwa upande wetu kama utawala taratibu zote tumesha zifata na mambo yote muhimu tumesha yatekeleza kwa maana tayari tickets zimeshapatikana na timu imekuwa kambini kuanzia mwanzo wa wiki hii na wamekuwa wanaendelea na mazoezi kila siku.”
“Timu itaondoka kesho alfajiri, mda wa safari utakuwa ni dakika 90 na watapata muda mrefu wa mapumziko jioni watafanya mazoezi kwenye uwanja utakaotumiwa kwa ajili ya mechi siku ya Jumapili.”
“Baada mechi timu itarejea Jumanne kwa ajili ya maandalizi kwa ajili ya mechi ya marudiano kikosi chote kipo kaminili ukiachilia mbali majeruhi wachache, watanzania wasiwe na wasiwasi mambo yote yanaendelea vizuri.”
Yanga itasafri na msafara wa jumla ya watu 30. Wachezaji 20, benchi la ufundi litakuwa na watu nane, muwakilishi mmoja kutoka TFF, na mjumbe wa kamati ya utendaji ndio atakuwa kiongozi wa msafara.

Mashabiki wa Stand United wanaokata tamaa, kocha amewapa neno…



Stand United inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Majimaji kwenye uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, kocha wa Stand Augustino Malindi amesema wamejipanga kuhakikisha wanapata ushindi kwenye mchezo huo.
“Tumejipanga kushinda mechi dhidi ya Majimaji, mimi nafikiri kwenye mpira huwa hakuna sababu kwamba kwa nini umepoteza inapofikia wakati unafungwa inabidi ukubali na inapotokea timu imeshinda ni sawa kwa sababu ndio mpira ulivyo ndio maana timu inafanya mazoezi.” – Augustino Malindi
“Kuna sababu nyingine ambazo hata ukiziongelea inakuwa sio, mechi yetu tuliyocheza Kagera mwamuzi hakuwa fair kwa upande wetu kwa sababu tulipata penati mbili lakini hatukupewa hali kadhalika fourth official akamtoa kocha wetu wa makipa na kuwapandisha jukwaani.”
“Tumeenda Tanga hali ikawa hivyohivyo, mechi ambazo tulikuwa tunaweza kushinda lakini tunashindwa kutokana na maamuzi ya ma-referee.”
“Mashabiki wetu wasikate tama, watupe sapoti kama walivyotupokea tulivyorudi kucheza na Yanga. Mwalimu amefanyia kazi safu ya ushambuliaji na ulinzi tunaingia kucheza na Majimaji tukiamini tutapata ushindi na kuibuka na pointi tatu.”


SAMATTA APIGA BAO MECHI YA MAHASIMU, GENK YAUA 3-0
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta amerejea uwanjani usiku wa jana na kuifungia KRC Genk bao la pili katika ushindi wa 3-0 dhidi ya mahasimu, Sint-Truiden katika mchezo wa Ligi Daraja la Kwanza A Uwanja wa Stayen, Sint-Truiden, St.-Trond.
Samatta aliyekuwa anacheza kwa mara ya kwanza tangu aumie mgongo Februari 1, alifunga bao lake dakika ya 39 kwa kichwa akimalizia krosi ya kiungo fundi wa Kispaniola, Alejandro Pozuelo Melero. 
Na Pozuelo alimsetia Samatta kufunga bao la pili, akitoka kufunga bao la kwanza yeye mwenyewe dakika ya 37, akimalizia kazi nzuri ya mshambuliaji chipukizi Mbelgiji, Siebe Schrijvers.
Mbwana Samatta akikimbia kushangilia baada ya kufunga bao lake jana

Bao la tatu la KRC Genk ambayo sasa inafikisha pointi 41 katika nafasi ya tano baada ya kucheza mechi 26, lilifungwa na kiungo wa kimataifa wa Ukraine, Ruslan Malinovskiy dakika ya 45. 
Februari 1 Samatta alicheza kwa dakika 23 tu kabla ya kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo akiiacha KRC Genk ikifungwa 1-0 na KV Oostende Uwanja Luminus Arena, Genk katika mchezo wa Kombe la Ubelgiji na kutolewa.
Jana Samatta alicheza mechi ya 41 tangu asajiliwe Genk Januari mwaka jana, 18 msimu uliopita na 23 msimu huu na kati ya hizo, ni michezo 22 tu ndiyo alianza, 10 msimu uliopita na 11 msimu huu.
Mechi 19 kati ya hizo alitokea benchi, nane msimu uliopita na 11 msimu huu, wakati 10 hakumaliza baada ya kutolewa, sita msimu uliopita na nne msimu huu huku akiwa amefunga jumla ya mabao 12, sita msimu huu na sita msimu uliopita.
Kikosi cha KRC Genk kilikuwa: Ryan, Uronen, Colley/Wouters dk82, Brabec, Castagne, Berge, Malinovskyi, Pozuelo/Boetius dk62 Trossard/Naranjo dk70, Writers na Samatta.
STVV:Pirard, Mechele, Peeters, Gerkens, Bagayoko/Dussaut dk63, Janssens/Boli dk45, Kotysch, Valdivia, Fernandes, Vetokele na Bolingoli/Ceballos dk45.

SIMBA KURUDI KILELENI LIGI KUU LEO?
SIMBA SC itajaribu kurejea kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara wakati itakapomenyana na Prisons ya Mbeya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo.
Timu hiyo ya kocha Mcameroon, Joseph Marius Omog itaingia kwenye mchezo wa leo ikihitaji ushindi tu ili kurejea kileleni mwa Ligi Kuu.
Na hiyo ni kwa sababu wapinzani wao katika mbio za ubingwa, Yanga SC hawatakuwa na mechi ya Ligi Kuu wikiendi hii kwa kuwa wamekwenda Comoro kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Na wakitoka kushinda 3-0 ugenini katika mechi iliyopita ya Ligi Kuu dhidi ya wenyeji Maji Maji mjini Songea, Simba wanajamini kabisa leo wataendeleza wimbi la ushindi.
Na bila shaka, kocha Omog anayesaidiwa na Mganda, Jackson Mayanja leo ataendelea kupanga safu kali ya ushambuliaji ya wakali watatu, Juma Luizio, Ibrahim Hajib na Mrundi Laudit Mavugo.  
Kwa ujumla Omog hatarijiwi kufanya mabadiliko makubwa kutoka kikosi kilichoifunga 3-0 Maji Maji Jumamosi Uwanja wa Maji Maji, Songea.
Na bila shaka langoni ataendelea kusimama Mghana Daniel Agyei, akisaidiwa na beki Mkongo Janvier Bokungu kulia, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ kushoto na katikati Mzimbabwe Method Mwanjali na Novatus Lufunga.
Viungo wanaweza kuendelea kucheza Muzamil Yassin, Said Ndemla na Shizza Kichuya. Simba SC inashika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu kwa pointi zake 48 baada ya kucheza mechi 21, ikiwa nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga wenye poinyi 49 za mechi 21.



Pamoja na kutofanya vizuri katika msimu uliopita, Manchester United imeshika namba moja katika mauzo ya jezi baada ya kuuza zaidi ya jezi milioni 2.8.




Mauzo ya jezi kwa mwaka 2016 yameshikwa na Man United huku wakifuatiwa na Real Madrid ya Hispania iliyouza zaidi ya jezi milioni 2.2.

FC Barcelona ya Hispania pia, imeuza jezi milioni 1.9 na kufuatiwa na Chelsea Chelsea iliyouza jezi milioni 1.6.



LISTI YA KLABU ZILIZOUZA SANA
1) Manchester United (2,850,000)
2) Real Madrid (2,290,000)
3) Barcelona (1,980,000)
4) Chelsea (1,650,000)
5) Bayern Munich (1,500,000)
6) Arsenal (1,225,000)
7) Juventus (850,000)
8) Liverpool (705,000)
9) Paris Saint-Germain (685,000)

10) AC Milan (650,000)

Jumatano, 18 Januari 2017

november 30/12



MAFUNZO YA VITENDO YAWA FURAHA KWA WANAFUNZI VYUONI

Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha,wakiwa katika mafunzo ya vitendo wakiwa darasani.


Wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari na utangazaji Arusha wametakiwa kujifunza masomo yao kwa vitendo ili kuongeza maarifa zaidi na kuleta ushindani katika soko la ajira pindi watakapoajiriwa.



Hayo yamesemwa na mkufunzi wa chuo hicho Bw;Steven Mulaki alipokuwa akihojiwa na SPIRITMWAMBA mapema leo mchana alipokuwa akiwafundisha wanafunzi wa darasa la Mt Ordizungwa.



Bw Mulaki ameongeza kwa kusema kuwa mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa vyuoni ni muhimu kwa kuwa watakapohitimu masomo yao itawasaidia kupata uzoefu watakapoajiriwa na taasisi au makampuni mbalimbali



Kwa upande wa wanafunzi wamefurahishwa na mafunzo hayo ambapo wengi wao wamemsifu mkufunzi huyo kwa kufundisha vizuri.




Kamanda Wa Polisi Mkoa Wa Singida Afariki Dunia, Mwili Kuagwa Leo Saa 11 Jioni Muhimbili

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) EX Peter Kakamba amefariki dunia alfajiri ya tarehe 30/11/2016 katika hospital ya taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.

Kakamba alizaliwa mwaka 1963 katika kijiji cha Kawajense Wilayani Mpanda, mkoa wa Katavi. Alisoma shule ya msingi Shanwe Kawajense  mwaka 1973 hadi 1980, Kidato cha kwanza hadi cha nne katika shule ya Sekondari Kantalamba mwaka 1981 hadi 1984 ambapo kidato cha tano na sita alisoma katika shule ya Sekondari Umbwe mkoani Kilimanjaro mwaka 1985 hadi 1987. Mwaka 1992 hadi 1994 alisoma Astashahada ya Sheria katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Marehemu alijiunga na Jeshi la Polisi mwaka 1988 ambapo katika utumishi wake alipandishwa vyeo mbalimbali ikiwemo Konstable wa Polisi (1989), Sagenti wa Polisi (1991), Mkaguzi Msaidizi wa Polisi (1997), Mkaguzi wa Polisi (2003), Mrakibu Msaidizi wa Polisi (2006), Mrakibu wa Polisi (2008), Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (2011), Kamishna Msaidizi wa Polisi (2015) na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (2016).
 
Baadhi ya nafasi alizowahi kushika ni pamoja na kuwa  Mwendesha Mashtaka wa Polisi katika mkoa wa Iringa, Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Mufindi, Afisa mnadhimu wa Polisi katika Mikoa ya Iringa na Geita, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa na mpaka anafariki alikuwa Kamanda wa Polisi katika mkoa wa Singida.
 
Kufuatia kifo hicho Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu anatoa pole kwa Maofisa, Wakaguzi,Askari, ndugu, jamaa na marafiki kwa Msiba huo.
Bwana alitoa na Bwana ametwaa,
Jina la Bwana lihimidiwe - Amen.

Imetolewa na:
Advera John Bulimba - ACP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Makao Makuu ya Polisi.        

Alhamisi, 12 Januari 2017

michezo alhamisi hii

 

 

 BPL-FUATILIA HAPA

TIMU YA BARCELONA YATINGA ROBO FAINALI YA COPA DEL REY

Luis Suarez amefunga goli la 100 katika michezo 120 akiwa na Barcelona wakati timu hiyo ikitinga robo fainali ya Copa del Rey kwa kuifunga Athletic Bilbao magoli 3-1.

Suarez alifunga goli katika kipindi cha kwanza kufuatia krosi ya Neymar, na katika kipindi cha pili Neymar akafunga goli la pili kwa mkwaju wa penati.

Athletico Bilbao walipata goli pekee lililofungwa na kichwa na mshambulia Saborit, hata hivyo Lionel Messi aliipatia Barcelona goli la tatu kwa shuti la mpira wa adhabu.
                       Luis Suarez akimalizia vyema mpira wa krosi iliyopigwa na Neymar
   Lionel Messi akipiga mpira wa adhabu ulioenda kujaa wavuni na kuipatia ushindi Barcelona
 

SOUTHAMPTON YAITUNGUA LIVERPOOL GOLI MOJA BILA MAJIBU

Timu ya Southampton imeanza vyema mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya kombe la EFL, kwa kupata ushindi inaostahili wa goli 1-0 didi ya Liverpool katika dimba la St Mary.

Goli la Southampton lilimaliziwa vyena na Nathan Redmond akipokea pasi ya Jay Rodriguez, na kuipatia ushindi muhimu kabla ya mchezo wa marudiano Anfield Januari 25.
                                   Nathan Redmond akijipinda na kuachia shuti lililojaa wavuni 
       Nathan Redmond akishika kichwa baada ya kukosa nafasi ya kufunga goli la pili 
 

Diamond akabidhiwa bendera ya taifa kuliwakilisha taifa AFCON 2017 nchini Gabon

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akimkabidhi bendera ya Taifa Mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye akiongea na wageni waalikwa pamoja na Waandishi wa Habari wakati wa hafla ya kumkabidhi bendera ya Taifa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon. Hafla hiyo imefanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa pamoja na Waandishi wa Habari wakifuatilia hotuba ya Waziri Nape Nnauye wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum akiongea na Waandishi wa Habari pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.
Balozi wa DSTV Bomba Bw. Lucas Mhuvile maarufu kama Joti akiongea na Waandishi wa Habari pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye, Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum pamoja na mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz wakiteta jambo kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati)  akimpongeza mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz wakiteta jambo kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon. Anayeshuhudia kushoto ni Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum
Mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz akimshukuru Waziri Nape Nnauye pamoja na Serikali kwa ujumla kwa mchango mkubwa inaotoa katika kukuza sekta ya Sanaa nchini wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.