AJTC VOICE FO VOICLESS

Alhamisi, 12 Januari 2017

michezo alhamisi hii

 

 

 BPL-FUATILIA HAPA

TIMU YA BARCELONA YATINGA ROBO FAINALI YA COPA DEL REY

Luis Suarez amefunga goli la 100 katika michezo 120 akiwa na Barcelona wakati timu hiyo ikitinga robo fainali ya Copa del Rey kwa kuifunga Athletic Bilbao magoli 3-1.

Suarez alifunga goli katika kipindi cha kwanza kufuatia krosi ya Neymar, na katika kipindi cha pili Neymar akafunga goli la pili kwa mkwaju wa penati.

Athletico Bilbao walipata goli pekee lililofungwa na kichwa na mshambulia Saborit, hata hivyo Lionel Messi aliipatia Barcelona goli la tatu kwa shuti la mpira wa adhabu.
                       Luis Suarez akimalizia vyema mpira wa krosi iliyopigwa na Neymar
   Lionel Messi akipiga mpira wa adhabu ulioenda kujaa wavuni na kuipatia ushindi Barcelona
 

SOUTHAMPTON YAITUNGUA LIVERPOOL GOLI MOJA BILA MAJIBU

Timu ya Southampton imeanza vyema mchezo wa kwanza wa nusu fainali ya kombe la EFL, kwa kupata ushindi inaostahili wa goli 1-0 didi ya Liverpool katika dimba la St Mary.

Goli la Southampton lilimaliziwa vyena na Nathan Redmond akipokea pasi ya Jay Rodriguez, na kuipatia ushindi muhimu kabla ya mchezo wa marudiano Anfield Januari 25.
                                   Nathan Redmond akijipinda na kuachia shuti lililojaa wavuni 
       Nathan Redmond akishika kichwa baada ya kukosa nafasi ya kufunga goli la pili 
 

Diamond akabidhiwa bendera ya taifa kuliwakilisha taifa AFCON 2017 nchini Gabon

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akimkabidhi bendera ya Taifa Mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz kwa ajili ya kwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye akiongea na wageni waalikwa pamoja na Waandishi wa Habari wakati wa hafla ya kumkabidhi bendera ya Taifa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon. Hafla hiyo imefanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Wageni waalikwa pamoja na Waandishi wa Habari wakifuatilia hotuba ya Waziri Nape Nnauye wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum akiongea na Waandishi wa Habari pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.
Balozi wa DSTV Bomba Bw. Lucas Mhuvile maarufu kama Joti akiongea na Waandishi wa Habari pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye, Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum pamoja na mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz wakiteta jambo kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati)  akimpongeza mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz wakiteta jambo kabla ya kuanza kwa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kushiriki katika Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon. Anayeshuhudia kushoto ni Mkurugenzi wa DSTV Multi Choice Tanzania Bw. Salum Salum
Mwanamuziki wa bongo fleva Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinumz akimshukuru Waziri Nape Nnauye pamoja na Serikali kwa ujumla kwa mchango mkubwa inaotoa katika kukuza sekta ya Sanaa nchini wakati wa hafla ya kukabidhi bendera ya Taifa kwa mwanamuziki huyo anayekwenda kuiwakilisha Tanzania kwenye Ufunguzi wa Mashindano ya AFCON 2017 yanayotarajiwa kufanyika nchini Gabon.iliyofanyika leo 11 Januari, 2017 Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni